Featured

Jaji Warioba: Siendi Dodoma katika makabidhiano ya katiba pendekezwa sababu soma zaidi hapa===>>


Wakati Katiba inayopendekezwa ikikabidhiwa kesho kwa Rais Jakaya Kikwete, Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema hata akialikwa katika sherehe hizo hatahudhuria kutokana na majukumu aliyonayo kwa sasa.

Jaji Warioba alisema angependa kuhudhuria sherehe hiyo ambayo pia itahudhuriwa na wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, wakuu wa mikoa, mabalozi na wageni mbalimbali, lakini kutokana na dharura aliyoipata haitawezekana.

Sherehe hiyo itafanyika mkoani Dodoma kesho na Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta atakabidhi nakala ya Katiba inayopendekezwa kwa Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein.

Katika hafla hiyo itakayofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri, wajumbe wa Bunge hilo walioshiriki mchakato huo kuanzia mwanzo mpaka mwisho watapewa vyeti.
Akizungumza na gazeti hili jana, Jaji Warioba alisema hadi jana hakuwa amepata mwaliko lakini hata kama akipewa hataweza kuhudhuria. “Siwezi kutoka nje ya Dar es Salaam kwa siku mbili tatu hizi kwa sababu nina dharura. Kama wakinialika nitawaomba radhi kwamba sitaweza kuhudhuria,” alisema.

Alipoulizwa iwapo Jaji Warioba ni miongoni mwa waalikwa katika sherehe hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Rehema Nchimbi alisema angetoa majibu leo kuhusu suala hilo lakini anaamini mkongwe huyo ni miongoni mwa viongozi wastaafu, hivyo kualikwa ni lazima.
Sherehe yenyewe
Mkuu huyo wa mkoa alisema sherehe hizo zitatanguliwa na dua ya kumshukuru Mungu kwa kumaliza Bunge hilo salama ambayo itafanyika leo mchana katika Bustani ya Mwalimu Nyerere.
Wageni wengine walioalikwa ni pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa dini na wengine wastaafu. “Hatuna uhakika na viongozi wengine kutoka nje ya nchi maana mwaliko umetoka kwa muda mfupi, lakini mabalozi waliopo nchini wote tumewaalika na makundi mengine yote kama wakulima, wasanii, wavuvi, wafugaji na kila anayeguswa na Katiba mwakilishi wake lazima atakuwapo,” alisema Dk Nchimbi.
Kuhusu orodha kamili ya waalikwa alisema: “Kesho (leo) naweza kuwa na majibu mazuri kwa kila kitu maana tunashirikiana na vyombo vingine katika kazi hii, kwa hiyo nitawaambia kwani vikao bado vinaendelea.”


Awali, Naibu Katibu wa lililokuwa Bunge la Katiba, Dk Thomas Kashililah alisema maandalizi ya sherehe hiyo yamefanyika chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu
Mbinu Za Kumfikisha Kileleni Mwanamke Mwenye Makalio Makubwa Kwa Haraka: BONYZA HAP CHNI
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip KUJUA SEHEMU 12 ZINAZOMPA RAHA MWNAMKE WAKATI WA TENDO BONYZA HAP CHNI
Newer Posts Older Posts
© Copyright RAHA ZA MAPENZI Published.. Blogger Templates
Back To Top